• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Tanzania Rural and Urban Roads Agency-TARURA
Tanzania Rural and Urban Roads Agency-TARURA

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Muundo wa Taasisi
    • Dira na Dhima
  • Miradi na Programu
    • Miradi iliyo kamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyochini ya Ununuzi
    • Project and Program
    • RISE - DEC 2020
  • Utawala
    • Kurugenzi ya Huduma na Uendeshaji
    • Kurugenzi ya Barabara za Vijijini
    • Kurugenzi ya Barabara za Mijini
    • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
    • Kitengo cha Huduma za Sheria
    • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
    • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
    • Kitengo cha udhibiti Ubora na Utafiti
    • Sehemu ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA)
    • Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu
    • Sehemu ya Mipango
    • Waratibu wa Mikoa
    • Mameneja wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Bajeti na Taarifa za Mapato
    • Fomu Mbalimbali
    • Majarida
    • Vipeperushi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video
    • Habari
    • Matukio
    • Maktaba ya Picha
  • Manunuzi
    • Taarifa ya Manunuzi
    • Zabuni za Wazi
    • Tuzo za Zabuni
  • Mitandao ya Barabara
    • Mitandao ya Barabara za Tarura
  • Mikoa
    • Waratibu wa Mikoa
    • Mameneja wa Halmashauri

TARURA YADHAMIRIA KUUNGANISHA WILAYA YA RUANGWA NA LIWALE

Posted on: November 28th, 2020

TARURA YADHAMIRIA KUUNGANISHA WILAYA YA RUANGWA NA LIWALE 

Na. Bebi Kapenya.

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), umeendelea kuboresha miundombinu ya barabara na madaraja katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi ikiwemo ujenzi wa daraja la Mto Mbwemkuru lenye urefu wa mita 75 linalojengwa katika barabara ya Chikwale hadi Liwale kwa gharama ya Shilingi Bilioni 4.5.

Meneja wa TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Mhandisi Mashaka Nalupi alisema mradi wa ujenzi wa daraja la Mto Mbwemkuru umetokana na mpango wa kuunganisha Wilaya ya Ruangwa na Wilaya ya Liwale kwa lengo la kurahisisha mawasiliano kwa wananchi wa maeneo hayo na kuwezesha shughuli zao za kiuchumi na kijamii kwa haraka.

“Wilaya hizi mbili ni maarufu sana katika kilimo cha korosho na ufuta, lakini pia wananchi wa vijiji vya Nangurugai, Mirui, Narungombe, Machang’anja na Chikwale watapata faida ya kiuchumi kwasababu mazao yao ya biashara yataweza kuvushwa kutoka upande wa Liwale kwenda Ruangwa ambapo kuna soko kubwa la mazao ya biashara pale Ruangwa mjini”, alisema Meneja huyo.

Mhandisi Nalupi alieleza kuwa hadi sasa TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa imeshapokea fedha Shilingi Bilioni 1.6 kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Mto Mbwemkuru na ujenzi utakuwa wa Awamu II ambapo Awamu ya I itakuwa ujenzi wa daraja lenyewe kwa kutumia Mkandarasi anaitwa Nyumbani Construction Company Limited kwa mkataba wa Bilioni 1.6 na Awamu ya II itakuwa ni ujenzi wa Makalavati makubwa upande wa Liwale kwa Mkandarasi anaitwa Lumo Cones ambaye ameshaingia mkataba na ujenzi unatarajia kuanza hivi karibuni.

Naye, Bw. Abdallah Nampundai Mkazi wa Ruangwa ameishukuru Serikali kwa ujenzi wa daraja hilo kwani utanufaisha wananchi kusafirisha mazao yao na kufanya biashara zao.

“Kwa sisi wafanyabiashara na wakulima tunatoa mazao yetu kutoka Ruangwa kupeleka Liwale na tunatoa Liwale kupeleka Kilwa hivyo kukamilika kwa daraja hili kutatusaidia sana kupitisha mazao yetu kwa urahisi”, alisema Bw. Nampundai.

Kwa upande wake, Bw. Leonard Abel Mkazi wa Kijiji cha Nangurugai ameishukuru TARURA kwa ujenzi wa daraja hilo kwani litakapokamilika litarahisisha usafiri kwasababu wanapata changamoto nyingi mvua ikinyesha ikiwemo kupoteza ndugu zao kwavile Mto huo una mamba wengi hasa kipindi cha mvua hivyo kukamilika kwake kutawasadia sana kwenye suala la usafiri.

Mbali na ujenzi daraja la mto Mbwemkuru, TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa imekamilisha ujenzi wa Barabara za Lami Ruangwa mjini jumla ya Kilomita 8.32 kwa fedha za Mfuko wa Barabara pamoja na fedha za mradi wa Mfuko wa Umoja wa Ulaya, pia wameweka taa za barabarani jumla ya Km 7.62 mradi uliofadhiliwa na REA (Wakala wa Umeme Vijijini).

Aidha, Meneja huyo alisema kuwa wameweza kuunganisha sehemu kubwa ya Mji wa Ruangwa kwa barabara za Lami ambapo imeweza kurahisisha mawasiliano kwa watumiaji wa barabara na kuimarisha shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa maeneo hayo kwavile biashara zimeendelea kufanyika hadi nyakati za usiku kwasababu ya uwepo wat aa za barabarani.

TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa inaendelea na kazi mbalimbali za kuboresha miundombinu ya barabara na madaraja ili kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii na kiuchumi kwa urahisi.

Matangazo

  • INVITATION FOR LOGO DESIGN COMPETITION November 12, 2020
  • SHINDANO LA KUANDAA NEMBO (LOGO) YA TARURA-KISWAHILI November 12, 2020
  • WALIOITWA KWENYE USAILI KADA YA UDEREVA TARURA MKOA WA TANGA November 06, 2020
  • KUITWA KWENYE USAILI-KIGOMA October 30, 2020
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TARURA WAHIMIZWA KUONGEZA KASI YA UTENDAJI KAZI

    December 17, 2020
  • TARURA WILAYANI LIWALE YATEKELEZA MIRADI YA AHADI ZA VIONGOZI

    December 10, 2020
  • TARURA YAPONGEZWA UJENZI WA DARAJA LA KANKWALE MKOANI RUKWA

    December 08, 2020
  • BILLION 7.4 ZATUMIKA KUING’ARISHA HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA

    December 07, 2020
  • Angalia zote

Video

Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Tarura Barua pepe za Watumishi

Tovuti Muhimu

  • Wakala wa Barabara
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • OR-TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Wizara ya Ujenzi uchukuzi na mawasiliano
  • Utumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Baraza la Mitihani
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Instragram_tarura
  • twitter_tarura

Waliotembelea duniani

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    TANZANIA RURAL AND URBAN ROADS AGENCY (TARURA),TARURA HOUSE GOVERNMENT CITY -MTUMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 11042, DODOMA

    Simu ya mezani: 026-2963846

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ceo@tarura.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Waliotembelea

StatCounter

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki @2017 TARURA. Haki zote zimehifadhiwa